Huruma za Mungu: Siri ya Kufuta Machozi Katika Safari ya Imani
"True stewardship begins not in the pocket, but in the courage to touch another's coffin of pain." — GDeBh HURUMA ZA MUNGU: Siri ya Kufuta Machozi Katika Safari ya Imani Na: Mwl. Challo GC "Bwana alipomwona alimuonea huruma, akamwambia, Usilie. Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichua wakasimama. Akasema, Kijana, nakuambia, Inuka." — Luka 7:13-14 Tafakari ya Andiko Kuu: Mungu Anayegusa 'Jeneza' Lako Katika andiko hili, Yesu hakuingia mji wa Naini kama mgeni anayepita; aliingia kwa majira ya Mungu. Alipokutana na msafara wa mazishi, aliona kile ambacho watu wengine walikiona kama "mwisho." Mjane huyu alikuwa amepoteza mtoto wake wa pekee—tegemeo lake, heshima yake, na furaha yake. Yesu alipoliona jeneza, hakubaki kimya. Huruma yake ilimfanya aingilie kati. Kumbuka, katika utamaduni wa Kiyahudi, kugusa jeneza lilikuwa tendo la kujitia unajisi kisherehe. Lakini Yesu, kwa sababu ya huruma zake, alikubali kuvuka mipaka ya kidini ili...